Acheni Acheni
- Anonymous
- Nov 18, 2023
- 1 min read
(Mwenyezi ameniumba, akanileta kati
yenu, niwakumbushe watu wake thamani
yenu duniani) x2 (Acheni acheni kufa
moyo, acheni acheni kukata tama.Yeye
aliyewaumba anaijua kazi yake) x2
Aliijua asili yenu hata kabla
hamjaumbwa, Ramani ya maisha yenu,
yote imo mikononi mwake, magonjwa
yanayowatesa na maumivu yasiyokoma,
ni mdogo kuliko yale aliyoyaponya mwenyewe
Hali mbaya ya kiuchumi, mlo mmoja madeni
mengi, ni njia ya kunyenyekea na kumpa
Mungu ukuu, misiba inayowaliza mnapofiwa
na ndugu zenu, ni njia ya wapendwa wenu
kwenda mbinguni wakafurahi
Maumivu ya kuonewa kudhulumiwa
kusingiziwa, ni nafasi ya kusamehe na
kuishi kwa utakatifu. Matatizo ya ndoa
zenu na migogoro ya familia, ni bahati
mmejaliwa ya kuishi kwa uvumilivu
Bebeni misalaba uyenu, nyamazeni
msinungunike huo ndio wokovu wenu
shikilieni msiachie

Comments