Ahadi za Mungu
- Thomas Joseph
- Mar 22, 2024
- 1 min read
Ahadi zako Mungu twajua ni zile zile na neno lako wewe haliwezi badilika
Tunafahamu wewe unatimiza yote haubagui wewe unatimiza kwa wote
Bwana zishushe ahadi zako kwetu Bwana zimimine neema zako kwetu nasi tutazipokea x2
Ulimuahidia Babu yetu Ibrahimu yeye na uzao wake baraka
Umetuahidia kutujalia memayo fedha na dhahabu vyote ni vyako
Furaha na amani hivyo vyote mali yako Bwana tukirimie twakusihi
Mwisho wa yote haya utujalie uzima, uzima uzima wa milele uzima uzima wa milele x4

Comments