Asubuhi
- Hymns
- Nov 6, 2023
- 1 min read
Bwana asubuhi kucha nitakuinua
Sauti yangu kuomba, nipate baraka.
Nakuomba roho yako niongozwe nayo;
Nifanye yanipasayo, na mapenzi yako.
Wanaokutegemea, U Mlinzi wao;
Matumaini wanayo, utayatimiza.
Na kwa wingi wa fadhili, Nyumbani mwako juu
Nitaingia na wimbo, Pale kusujudu.

Comments