top of page

Bwana Kazi Zako

Ee Bwana kazi zako zitakushukuru (wewe) na wacha Mungu wako watakuhimidi x2

Watasema aleluya wataimba nyimbo nzuri, watacheza kwa furaha mbele zako Bwana. Kwa uzuri wako wewe na fadhili zako wewe watatoa shukrani mbele zakoo ee Bwana


Ee Bwana kwa uwema umejitolea (wewe) ukatupa chakula chako cha mbinguni x2


Ee Bwana Mungu wangu nitakushukuru (wewe) nitatoa dhabihu ya kukushukuru x2


Ee Bwana kweli mimi ni mtumishi wako (wewe) mtumishi na mwana mjakazi wako x2

Comments

Rated 0 out of 5 stars.
No ratings yet

Add a rating

Recent Posts

bottom of page