top of page

Bwana Nikufananishe na Nini

Updated: Dec 25, 2023


Bwana nikufananishe na nini, au nikufananishe na nani, pendo lako kwangu ni la ajabu, ndio sababu ya furaha yangu x2

  1. Kwa kuwa Bwana ulinijua, tangu tumboni mwa mama yangu, ukanitunza kwa upendo, ukanijaza pendo lako.

  2. Nilipokuwa kwenye mateso, nilifikiri umeniacha, mawazo yangu ya kitoto, sikutambua pendo lako.

  3. Kwangu ulijifunua Bwana, moyo wangu ulikutambua, matendo mengi yenye nguvu, uliyotenda mbele yangu.

  4. Nakiri mbele yako ee Bwana hakuna atakaye nitenga, na pendo lako, lenye nguvu, pendo lisilo na kipimo.

Comments

Rated 0 out of 5 stars.
No ratings yet

Add a rating

Recent Posts

bottom of page