top of page

Bwana ninakuhitaji!

  • Hymns
  • Nov 7, 2023
  • 1 min read

Bwana ninakuhitaji! Nimpofu, maskini;

Unishike mkononi, Kwako napata nguvu.


Kila saa, kila saa Bwana ninakuhitaji;

Kila saa, kila saa, Unilinde kila saa.


Univike na mavazi Ya usikivu wako;

Nguo zangu ni machafu, Nazitamani zako.


Wewe ukiniongoza Nitakwenda salama;

Nenda nami siku zote, U nuru na uzima.


Na ikiwa m-beleni Sehemu yangu ngumu,

Au ikiwa furaha, Unilinde kila saa.

Comments

Rated 0 out of 5 stars.
No ratings yet

Add a rating

Recent Posts

bottom of page