top of page

Mungu Wangu Mbona Umeniacha

Updated: Oct 22, 2023


Mungu wangu, Mungu wangu mbona umeniacha

  1. Wote wanionao huncheka sana, Hunifyonya watikisa vichwa vyao husema hutegemea Bwana na amponye, Na amwokoe sasa maana apendezwa na yeye

  2. Kwa maana mbwa wamenizunguka, Kusanyiko la waovu wamenisonga Yamenizua mikono na miguu, Naweza kuihesabu mifupa

  3. Wanagawanya nguo zangu, Na vazi wanalipigia kura Nawe usiwe mbali, Ee Mungu wangu fanya haraka kunisaidia

  4. Nitalihubiri jina lako kwa ndugu zangu, Katikati ya kusanyiko nitakusifu Ninyi mnaomcha Bwana, msifuni, Enyi nyote mlio wazao wa Yakobo mtukuzeni.

Comments

Rated 0 out of 5 stars.
No ratings yet

Add a rating

Recent Posts

bottom of page