top of page

Mwanga Umo Moyoni

  • Hymns
  • Nov 6, 2023
  • 1 min read

Mlimani pana mwanga, Mwanga wa jua zuri

Shambani na baharini Jua tukufu liko;

Mwanga uliyo mkubwa Umo moyoni mwangu,

Kwa kuwa Yesu alipo Hapa pana mwangaza.


Mwangaza ulio mzuri. Mwanga umo moyoni;

Akiwapo Bwana Yesu Pana mwanga moyoni.


Kama mavazi kikuu, Ninavua huzuni:

Nguo nzuri za kuvaa, Umenipa za kuvaa.

Nakuandama rohoni Hatanyumba ya juu

Iliyopambwa vizuri Katika pendo lako.


Ulinikomboa Yesu; Maisha yangu, mali,

Vyote nivyako, Mwokozi Daima nikusifu.

Nakuandama rohoni Hatanyumba ya juu

Iliyopambwa vizuri Katika pendo lako.

Comments

Rated 0 out of 5 stars.
No ratings yet

Add a rating

Recent Posts

bottom of page