Naamini
- Hymns
- Nov 6, 2023
- 1 min read
Baba sina msaada Ila kwako pekee:
Kama kwangu ungefichwa, Nifanyeje, Baba?
Sasa hivi naamini Yesu alikufa,
Alimwaga damu yake, Nitoke dhambini.
Naamini mwana wako Nipe nguvu zako:
Nijazie mahitaji, Katika saa hii.
Ni furaha gani kwangu Kukuona uso!
Nijue sauti yako, Nipate neema.

Comments