top of page

Nataka Imani Hii

  • Hymns
  • Nov 6, 2023
  • 1 min read

Nataka Imani hii: Imani imara,

Ambayo haitetemi Kitu chote

Wakati wa shida,

Wakati wa shida.


Isiyonung`unika Huzuni, taabu;

Lakini katika saa ya matata

Humwamini Mungu,

Humwamini Mungu.


Imani inayo ng`aa katika tufani;

Isiyoogopa giza, wala shida,

Njaa na Hatari,

Njaa na hatari.


Haiogopi dunia, Kudharau kwake;

Haiangushwi na hila, na uwongo

Dhambi na ogofyo,

Dhambi na ogofyo.


Bwana, nipe imani hii, Hivi nitaweza

Kuonja hapa chini ulimwenguni,

Kurithi furaha,

Kurithi furaha.

Comments

Rated 0 out of 5 stars.
No ratings yet

Add a rating

Recent Posts

bottom of page