top of page

Nena Mungu

  • Hymns
  • Nov 6, 2023
  • 1 min read

Nena rohoni Yesu, Nena kwa upole

Sema kwangu kwa pendo, ‘Huachwi upweke.‘

Fungua moyo wangu, Nisikie mara;

Jaza roho na sifa, Sifa zako Bwana.


Kila siku unene, Vile kwa upole,

Nong`oneza kwa pole wa pendo:

‘Daima utashinda, Uhuru ni wako.‘

Nisikie maneno; ‘Huachwi upweke.‘


Nena kwa wana wako, waonyeshe njia,

Wajaze kwa furaha, Fundisha kuomba;

Wajifunze kutoa Maisha kamili,

Wahimize ufalme, Tumwone mwokozi.


Nena kama zamani, Ulipoitoa

Sheria takatifu: Niiweke pia;

Nipate kutukuza Wewe Mungu wangu,

Mapenzi yoko tena, Daima kusifu.

Comments

Rated 0 out of 5 stars.
No ratings yet

Add a rating

Recent Posts

bottom of page