top of page

Ni Siku ya Furaha

  • Hymns
  • Nov 6, 2023
  • 1 min read

Ni siku ya furaha, ni siku ya nuru;

Nasi twaona raha, Kuja kushukuru;

Leo watu wa Mungu, wadogo, wakubwa,

Hukaribia mbingu, lilipo baraka.


Leo, ndiyo bandari, nasi twawasili,

Hiyo bustani nzuri, ya nyingi fadhili:

Kijito cha baridi kimefanya ziwa,

Na kiu ikizidi, twanywa maridhawa.


Leo ngazi na iwe ifakayo juu,

Mawazo na yasiwe ya duniani tu;

Leo ni kujilisha chakula cha mbingu,

Na kujifurahisha kwa mambo ya Mungu.

Comments

Rated 0 out of 5 stars.
No ratings yet

Add a rating

Recent Posts

bottom of page