Nilipotoka kabisa
- Hymns
- Nov 7, 2023
- 1 min read
Nilipotoka kabisa, sasa narudi;
Nikakawia dhambini, Bwana narudi.
Narudi nyumbani: daima kwako.
Kwa upendo nipokee: Naja nyumbani.
Nikasusurika sana, sasa narudi;
Mwenye uchungu natubu, Bwana narudi.
Nimechoka maovuni, sasa narudi;
Pendo lako lanivuta, Bwana narudi.
Ndilo tumaini langu, sasa narudi;
Yesu alinifilia, Bwana narudi.
Damu yake yanitosha, sasa narudi;
Unioshe kenyekenye, Bwana narudi.

Comments