Nisamehe Bwana
- Conrad Mghanga
- Oct 22, 2023
- 1 min read
Updated: Dec 25, 2023
Nisamehe Bwana mimi mtumishi wako, naja mbele yako naja na sala yangu, ninanyenyekea chini ya miguu yako, unitakase kwa makosa yangu yote
Sistahili mimi kuikaribia meza, wala hata kunena jambo lolote, nimejuta sana naomba huruma yako, unipokee mimi mtumishi wako
Ninapokuomba Bwana unisikilize, mahangaiko ya dunia mengi sana, yamenisonga kushoto hata kulia, mbele mbele na nyuma mimi sioni kitu
Ndugu zangu nao wananichekelea, ninapopambana na hali hali zangu, hivyo tumaini langu naliweka kwako, njoo hima Bwana wangu uniokoe

Comments