top of page

Nitakuandama Kote

  • Hymns
  • Nov 7, 2023
  • 1 min read

Nitakuandama kote, nitakapoagizwa

Wewe ukiniongoza nami nitaandama.


Nitakuandama kote, naam, ulinifia;

Kwa neema yako Bwana napenda kuandama.


Njia ijapoparuza kwa miiba na fujo,

Ulitangulia mbele nami nitaandama.


Nijapokuta taabu na majaribu kote,

Nakumbuka shida yako, nami nitaandama.


Nijapoona ukiwa na mateso makali,

Wewe uliyatikiza nami nitaandama.


Ijapo wanipeleka vilindini mwa giza,

Wewe uliyetikiza nami nitaandama.

Comments

Rated 0 out of 5 stars.
No ratings yet

Add a rating

Recent Posts

bottom of page