top of page

Zitakuwa Nyota Tajini

  • Hymns
  • Nov 6, 2023
  • 1 min read

Leo nina fikiria nchi nzuri Ninayotaka kuiona;

Nisimamapo karibu na Mwokozi, Tajini zitakuwa nyota?


Sijui tajini mwangu kama nyota

Zitang`aa kila wakati!

Nitakapoamka katika majumba

Zitakuwa nyota Tajini?


Kwa nguvu za Bwana nitafanya kazi, Nitavuta roho za watu,

Ili niwe na nyota katika taji, Bwana anapotupa tunu.


Nitakuwa na furaha nikimwona, Kuweka miguuni pake

Watu walio vutwa kwa ajili ya Kazi yangu na Roho yake.

Comments

Rated 0 out of 5 stars.
No ratings yet

Add a rating

Recent Posts

bottom of page